
Gazeti la ngono maalumu kwaajili ya watu wasioona limezinduliwa nchini Kanada likiwa na picha za ngono na hadithi za ngono.
Gazeti hilo linatumia herufi za maandishi ya wasioona kuchora picha za wanawake na wanaume wakiwa uchi huku picha hizo zikiambatana na maandishi yenye stori za ngono ngono.
Gazeti hilo limezinduliwa wiki hii nchini Kanada likiwa ni wazo la Lisa Murphy na gazeti hilo linakwenda kwa jina la "Tactile Minds".
Gazeti linalodaiwa kuwa la kwanza duniani la ngono kwaajili ya watu wasioona linauzwa bei ghali sana sawa na Tsh. Laki tatu.
Lisa alisema kuwa aliamua kuanzisha gazeti hilo ili kuziba pengo kwenye soko la ngono ambapo watu wasioona wameachwa mbali.
"Hakuna kitabu cha picha za ngono kwaajili ya wasioona", alisema Lisa.
"Tunafungua uwanja mpya, Jarida la Playboy lilikuwa na maandishi ya Braille lakini halikuwa na picha za ngono"
Katika miaka ya kati ya mwaka 1970 na 1985, Playboy walichapisha baadhi ya nakala za gazeti lao maarufu la Playboy katika maandishi ya braille lakini hakukuwa na picha.
Lisa alisema kuwa nakala yao ya kwanza ya gazeti la ngono kwaajili ya wasioona lina jumla ya picha 17 zilizochorwa kwa kutumia maandishi ya Braille.
Lisa aliendelea kusema kuwa watu wasioona watavuta hisia zao kwa kuzipapasa picha hizo zilizochorwa kwa ustadi mkubwa.






